Tuesday, June 21, 2016

TAARIFA KWA UMMA





YAH: KUSIKILIZA KERO NA KUPOKEA MAONI MBALIMBALI YA WANANCHI KUHUSU HUDUMA ZA HALI YA HEWA NCHINI.
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imeandaa siku ya Alhamis, saa 3 asubuhi hadi saa 8 mchana, Tarehe 23 Juni 2016 ili kusikiliza kero sambamba na kupokea maoni mbalimbali ya uboreshaji wa huduma za hali ya hewa nchini. Kazi hii  itafanyika katika ukumbi wa Mikutano, ghorofa ya tatu, Ubungo Plaza-Makao Makuu ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Kazi hii ni utekelezaji wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma nchini kwa mwaka 2016. 
‘Wananchi wote mnakaribishwa’
IMETOLEWA NA: OFISI YA UHUSIANO- MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...