Tuesday, March 8, 2016

KATIBU TAWALA WA WILAYA YA NYAMAGANA MKOANI MWANZA AWATAKA WANAHABARI KUTUMIA FURSA YA MAFUNZO YA EL-NINO NA ATHARI ZAKE KWA KIPINDI CHA UTABIRI WA MSIMU WA MVUA ZA VULI 2015 KAMA CHACHU YA UBORESHAJI WA ELIMU KWA JAMII.



Katibu tawala wa Wilaya ya Nyamagana Bibi Mayala amewataka wanahabari kutumia fursa ya mafunzo ya El Nino na athari zake katika msimu wa VULI katika kuboresha elimu kwa jamii kuhusu athari za El Nino nchini. Bibi Mayala aliyasema hayo wakati akifungua warsha ya wanahabari iliyofanyika Jijini Mwanza, tarehe 02 Februari 2016. Aidha, aliwapongeza TMA kwa jitihada zao kubwa za kuelimisha wanahabari kwa kuwa vyombo vya habari ni sekta muhimu katika kufikisha taarifa za hali ya hewa kwa wananchi.

Katika warsha hiyo Dkt. Kijazi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA alisema  warsha hiyo ni muhimu kwani itawawezesha wana habari kuwa na uelewa mkubwa wa taarifa za hali ya hewa na hivyo kuzisamabaza kwa usahihi zaidi. Aidha aliwashukuru wana habari kwa kuhuduria warsha hiyo na ushirikiano wanaoutoa katika kuhakikisha kwamba taarifa zinazotolewa na TMA zinawafikia wadau kwa wakati.  Dkt. Kijazi aliwashukuru wafadhili wa warsha hiyo ambao ni Serikali ya Norway kupitia Shirika la Hali ya Hewa ulimwenguni.

Kwa upande wa wanahabari, Bi. Theopista Nsanzugwanko kutoka gazeti la Habari Leo alisema semina hii itasaidia waandishi wa habari kuweza kujifunza masuala mbalimbali kuhusu mifumo ya hali ya hewa na kuwezesha kuandika  habari kwa usahihi na kusaidia jamii kutumia vema taarifa za hali ya hewa. Pia itawezesha jamii kupata elimu ya kukabiliana na madhara ya mvua za El Nino ili kupunguza madhara kwa jamii ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za tahadhari kwa usahihi zaidi.

TMA imekuwa ikiandaa warsha mbalimbali kwa wadau mbalimbali wakiwemo wanahabari katika mwendelezo wa utoaji elimu ya sayansi ya hali ya hewa pamoja na kudumisha ushirikiano baina ya Mamlaka na watumiaji wa taarifa za hali ya hewa ambao ni wadau kutoka sekta mbalimbali. Warsha hiyo imejumuisha wanahabari kutoka vyombo mbali mbali vya habari hapa nchini ambao wako Dar es Salaam na Mwanza.

IMETOLEWA NA MONICA MUTONI; AFISA UHUSIANO, MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...