Saturday, November 29, 2014

HALI YA HEWA YAENDELEA KUWANOA WATAALAMU WAKE KATIKA KUKIDHI VIWANGO VYA SHIRIKA LA HALI YA HEWA DUNIANI (WMO)




Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi ambaye pia alikuwa mgeni rasmi akizungumza na wahitimu wa mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma



Mwakilishi wa wahitimu Bi. Pamela Levira akisoma risala ya wahitimu kwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma

Mgeni rasmi, Mkurugenzi Mkuu wa TMA Dkt. Agnes Kijazi katika picha ya pamoja na wahitimu wa mafunzo ya huduma za hali ya hewa kwa ajili ya usafiri wa anga kutoka Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma,Kulia kwake mwenye tai nyekundu ni Mkuu wa Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma Bw. Joseph Aliba


Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini iliendesha mafunzo ya hali ya hewa kwaajili ya usafiri wa anga ‘Aeronautical Meteorology’. Mafunzo haya yalikuwa yakiendeshwa chini ya Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma ikiwa ni kuhakikisha wafanyakazi wa Mamlaka ya hali ya Hewa (TMA) kwa upande wa huduma za hali ya hewa kwa usafiri wa anga wanakidhi vigezo vilivyowekwa na WMO. Mafunzo haya ni ya pili kutolewa hapa nchini kupitia Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma.
Akifunga mafunzo hayo, Mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya Kozi ya Hali ya Hewa kwa ajili ua Usafiri wa Anga; Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt Agnes Kijazi alimpongeza Mkuu wa Chuo kwa kufanikisha kuendesha mafunzo hayo kwa mara ya pili ambayo ni moja ya utekelezaji wa vigezo vilivyowekwa kimataifa na WMO. ‘Kuendesha mafunzo haya kutawezesha Mamlaka kuwa na wataalamu wa kutosha wanaokubalika kimataifa kutoa huduma za hali ya hewa kwaajili ya usafiri wa anga, hivyo Mamlaka itakuwa imefikia viwango vilivyowekwa na Shirika la Hali ya Hewa Duniani, vinavyozitaka taasisi za hali ya hewa duniani kuwa na na wataalamu wenye shahada ya hali ya hewa na ujuzi unaotakiwa kwaajili ya kutoa huduma katika usafiri wa anga’Alisema Dk. Kijazi. Aidha aliwataka wahitimu kutumia ujuzi waliopata ili kufanya kazi kwa ufanisi na hviyo kuchangia katika maendeleo ya taifa.
Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha hali ya hewa Kigoma Bwana Joseph Aliba alisema Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma kimepata usajili wa kudumu toka NACTE na waalimu wote wamesajiliwa na NACTE.
Akiongea kwa niaba ya wahitimu Bi Pamela Levira ameishukuru Mamlaka kwa kuwajengea uwezo  wa kufanya kazi kwa kujiamini katika kutoa huduma za hali hewa katika sekta ya usafiri wa anga.
Chuo cha Hali ya Hewa Kigoma  ni chuo pekee Tanzania kinachotoa elimu ya ngazi ya cheti na diploma kwa taalamu ya hali ya hewa. Chuo kimepata usajili wa NACTE kwa leseni ya kuendesha mafunzo ya nje ya mipaka ya nchi ‘cross boarder license’.
Imetolewa na : Monica Mutoni Ofisa Uhusiano- Mamlaka ya Hali ya Hewa

No comments:

Post a Comment

Featured Post

DKT. KIJAZI: KIWANGO CHA USAHIHI WA UTABIRI WA MSIMU WA VULI 2019 KIWE CHA JUU ZAIDI.

Mkurugenzi mkuu wa TMA na Makamu wa Tatu wa Rais wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani Dkt. Agnes Kijazi (katikati mwenye suti nyeusi) waka...